Saturday, May 3, 2008

AKASEMA, NITAWEZAJE KUELEWA?

2866 - Swahili

Matendo 8:26-40

26. Malaika wa Bwana akasema na Filipo, akamwambia, Ondoka ukaende upande wa kusini hata njia ile itelemkayo kutoka Yerusalemu kwenda Gaza; nayo ni jangwa.
27. Naye akaondoka, akaenda; mara akamwona mtu wa Kushi, towashi, mwenye mamlaka chini ya Kandake malkia wa Kushi, aliyewekwa juu ya hazina yake yote;
28. Naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu, akawa akirejea, ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya.
29. Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo.
30. Basi Filipo akaenda mbio, akamsikia anasoma chuo cha nabii Isaya; akanena, Je!
31. Yamekuela haya unayosoma? Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye.
32. Na fungu la Maandiko alilokuwa akilisoma ni hili, Aliongozwa kwenda machinjoni kama kondoo, Na kama vile mwana-kondoo alivyo kimya mbele yake amkataye manyoya, Vivyo hivyo yeye naye hafunui kinywa chake.
33. Katika kujidhili kwake hukumu yake iliondolewa. Ni nani atakayeeleza kizazi chake? Kwa maana uzima wake umeondolewa katika nchi.
34. Yule tswashi akamjibu Filipo, akasema, Nakuomba, nabii huyu asema maneno haya kwa habari ya nami; ni habari zake mwenyewe au za mtu mwingine?
35. Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.
36. Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; Ni nini kinachonizuia nisibatizwe?
37. Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.
38. Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote mawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.
39. Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashiasimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.
40. Lakini Filipo akaonekana katika Azoto, na alipokuwa akipita akahubiri Injili katika miji hata akafika Kaisaria.

No comments: